Mwimbaji nyota wa muziki wa Injili nchini, Rose Muhando.
Akizungumza kutoka Dodoma yalipo makazi ya mwimbaji huyo, mmoja wa watu wake wa karibu aliyeomba hifadhi ya jina lake, alisema hatua ya Msama kutangaza kutofanya naye kazi, limekuwa pigo kwake kwani ndiye aliyekuwa kiongozi na mwokozi wake wa mambo mengi ya kikazi na binafsi.
Meneja wa Rose Mhando, Alex Msama.
“Anaweweseka kwa kweli na hajui la kufanya, Msama ndiye alikuwa msaada wake mkubwa kwa kila kitu kuhusiana na muziki japo kwa sasa amekuwa hataki hata kumsikia Rose,” alisema mtu huyo.
Rose alipigiwa kutaka kusikia kutoka kwake, lakini simu yake iliita bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi ulionyeshwa kupokelewa bila majibu. Msama alipoulizwa kuhusu kilio cha msanii huyo alisema yeye ameshatoa msimamo wake na unaeleweka.
Maskini Rose Muhando Apata Pigo Lingine Tena
Reviewed by habari motto
on
8:33 AM
Rating: