Kikosi cha Skylight Band kikiongozwa na mkongwe wa muziki wa Live Band, Joniko Flower (kushoto) kutoa burudani kwa mashabiki wake ndani ya viwanja vya Leaders Club kwenye tamasha la Nyama Choma lilifanyika mwishoni mwa wiki. Kutoka kulia ni Sam Mapenzi, Aneth Kushaba AK47 pamoja na Sony Masamba.
Swagga za Skylight Band hii inafahamika kama "Mashauzi" mkongwe Joniko Flower akiwasebenesha mashabiki wake ( hawapo pichani).
Asali ya warembo Sam Mapenzi akifanya yake jukwaani kwenye tamasha la Nyama Choma ndani ya viwanja vya Leaders Club.
Watu weweeeeeeee yani ni full mzuka...pole kwa uliyekosa burudani ya aina yake ndani ya Leaders Club.
Majembe ya Skylight Band yakiongozwa na Sony Masamba (katikati) kutoa burudani kwenye tamasha la Nyama Choma ndani ya viwanja vya Leaders Club. Kushoto ni Joniko Flower na kulia ni Sam Mapenzi.
Warembo wakijinafasi ndani ya Leaders Club kwenye tamasha la Nyama Choma huku Skylight Band ikitoa burudani.
Mashabiki wa Skylight Band wakiendelea kupata burudani huku wengine wakirekodi kumbukumbu ya burudani hiyo kwenye simu zao.
Idrissa Drums na Moses Kinanda wakipika muziki mzuri kuhakikisha walaji wa burudani ya Skylight Band wanashiba.
Pale raha ya burudani ya Skylight Band inapokolea ni kama hivi.....
John Music akifanya yake jukwaani huku akipewa sapoti na Ashura Kitenge, Baby pamoja na Sony Masamba.
SKYLIGHT Band Yaisindikiza Nyama Choma Festivl Kiivi...
Reviewed by habari motto
on
10:34 AM
Rating: