Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo, alithibitisha leo kutokea kwa ajali hiyo majira ya mchana na kupoteza uhai wa watu wawili ambao mwanaume mmoja na mwingine ni mwanamke na pia kujeruhi wengine 48 katika eneo la ndani ya hifadhi ya taifa ya Mikumi , barabara kuu ya Morogoro- Iringa.
Kwa mujibu wa Kamanda huyo, kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa basi hilo ambaye alitaka kulipita gari lililokuwa mbele yake, bila kuchukua tahadhari na alipoona kuna gari jingine likija kutoka upande wa Iringa aliamua kutanua upande wake zaidi na kujikuta likiacha njia na kupindula mara tatu .
Hata hivyo alisema baada ya kutokea kwa ajali hiyo , dereva wa basi alikimbia eneo hilo na anatafutwa na Polisi, ambapo majeruhi hao 48 , kati yao 12 wakiwemo wanawake sita na wanaume sita wamelazwa katika hospitali ya Misheni ya St Kizito ya Mikumi na wanaendelea vizuri.
Ajali Nyingie Yaua Mikumi
Reviewed by habari motto
on
9:17 PM
Rating:
![Ajali Nyingie Yaua Mikumi](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhsSIoGv1mCY-7m8SHoveITFcSp6CauDFOFfuvo-zajIqc3CmrUnXa4sT_6VKHJp-SDJ0-pf7BfrobamAXJ4-2cQEa7Ux0SeGOmfh-vlOXZIGnPMrOdyT99SXuDkUH9Pz0fTMuRzvc_lrq8/s72-c/IMG-20150409-WA0187.jpg)