Utawala Wa Jadi Unavyoona Mwenendo Wa Serikali.



KIONGOZI wa machifu wa kindali Wilayani Ileje , Chifu Etisoni Musomba amempongeza Rais John Pombe Magufuli kwa utendaji wake tangu alipochaguliwa kuongoza taifa hili.

Chief Musomba amesema hayo katika mahojiano maalum na Globu ya jamii juu ya namna gani utawala wa jadi unavyoona mwenendo wa serikali.

“Kiukweli kwa sasa hali ni nzuri maana kumekuwa na heshima ya kutosha hata watumishi wa serikali huku vijijini tumewaona wakifanya kazi kwa bidii kutokana na kuogopa kufukuzwa tofauti na awali ambapo walikuwa wanafanya wanavyotaka na machifu tulipokemea tulidharauriwa” amesema Chief Musomba.

Chief Musomba ameongeza kuwa vijiji vimekuwa  na amani sana,watoto wanapata elimu bure na wazazi hawasumbuliwi kuhusu fedha za ada wala michango mengine iliyokuwa kero kwao.

Amesema kuwa hapo awali wazazi walilazimika kuuza mifugo yao na kuingia katika umaskini mkubwa kutokana na kulipia Ada za watoto wao pindi wanapochaguliwa kwenda Sekondari bali kwa sasa fedha kidogo wanazopata kutokana na uuzaji wa mazo zinawatosha kujikimu katika kutatu matatizo ya watoto wa shule.

kwa hisani ya Humphrey Shao,Globu ya Jamii-ILEJE  
Utawala Wa Jadi Unavyoona Mwenendo Wa Serikali. Utawala Wa Jadi Unavyoona Mwenendo Wa Serikali. Reviewed by habari motto on 12:57 PM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.