“Jamani maisha yangu kwa sasa ni magumu kwani siwezi kufanya kazi yoyote na sina msaada na kwenye muziki sijaona faida yoyote labda ya nguo tu, kwamba nilizoea kuvaa madela na kanzu sasa nina suruali,” alisema Bi Cheka kwa machungu.Alisema anasikitishwa na maisha yake kwani kutokana na umaarufu wake, mtaani kwao anaonekana kama mtu mwenye uwezo, wakati siyo kweli kwani anaishi kwenye nyumba ya tembe katikati ya nyumba nzuri.
“Kuhusu malipo makubwa kuwahi kupata ni shilingi laki tatu nilizolipwa kwenye shoo ya Fiesta mwaka juzi, hizo ndizo hela kubwa niliyowahi kupata katika muziki.”Gazeti hili lilimtafuta Fella ambaye alikiri Bi. Cheka kuumwa, akisema anasumbuliwa na magonjwa ya uzee na kwamba ahadi yake ya kumsaidia kujenga nyumba imeishia kwenye mchango wake wa matofari.
“Mimi kama Fella nimesaidia ninapoweza, nimemchangia matofari kidogo, kwa hiyo watanzania wenzangu nao tuungane tumchangie ili aweze kurekebisha kibanda chake,” alisema.
Global Publishers inaanzisha kampeni maalum ya kumsaidia na hivyo inawaomba watanzania kumchangia msanii huyu ili apate nyumba nzuri na matibabu yake. Ili kumsaidia tuma fedha kwenye namba 0654-880707 ambayo itasimamiwa na kampuni.
Haya Ndiyo Maisha Duni Ya Msanii Bi.C heka..Yanasikitisha Sana
Reviewed by habari motto
on
12:06 PM
Rating: