Nyota: Neymar alifunga magoli mawili dhidi ya Cameroon
katika mchezo wa mwisho wa kundi A.
TIMU ya Taifa ya Brazil imefuzu hatua ya 16 ya kombe la
dunia baada ya kuifunga Cameroon mabao 4-1.
Mshambuliaji hatari, Neymar alifunga mabao mawili katika
dakika ya 17 na 34′,, huku mawili yakifungwa na Fred katika dakika
ya 49 na Fernandinho dakika ya 84′.
Bao la kujifutia machozi kwa Cameroon lilifungwa na Joel
Matip katika dakika ya 26 kipindi cha kwanza.
Hata hivyo aina ya mpira wa Brazil wa mwaka 2014 una
mapungufu na unaweza kudhani hawatafanikiwa kufika mbali zaidi katika michuano
hii.
Lakini Neymar anaoonekana kuipa nguvu zaidi na kubeba
michuano hii begani mwake.
Mchezaji mmoja anaweza kuiwezesha timu kutwaa ubingwa?
Labda hapana, lakini Neymar alifanya kazi nzuri katika
mchezo huo kuhakikisha timu yake inamaliza vizuri mechi ya mwisho ya makundi.
Nyota kinda wa Brazil, Neymar akifunga bao la kuongoza
katika dakika ya 17
Hapa chini ni vikosi vya timu zote
na viwango vya wachezaji. Alama ni chini ya 10.
Kikosi cha Cameroon: Itandje 6; Nyom 5.5, Nkoulou 5.5, Matip 6, Bedimo 5; Mbia
6, Nguemo 6, Enoh 6.5; Choupo Moting 6 (Makoun 80, 5.5), Aboubakar 5.5 (Webo
71, 6), Moukandjo 6 (Salli 57, 5).
Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Feudjou, Assou-Ekotto, Djeugoue, Nounkeu, Eto’o, Chedjou, Webo, Fabrice, N’Djock.
Kadi ya njano: Enoh, Mbia
Mfungaji wa goli: Matip 26′
Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Feudjou, Assou-Ekotto, Djeugoue, Nounkeu, Eto’o, Chedjou, Webo, Fabrice, N’Djock.
Kadi ya njano: Enoh, Mbia
Mfungaji wa goli: Matip 26′
Kikosi cha Brazil: Julio Cesar 6; Alves 6, Silva 6, Luiz 6, Marcelo 5.5;
Paulinho 5 (Fernandinho 45, 7.5), Luiz Gustavo 6.5, Oscar 6; Hulk 6 (Ramires
63, 5.5), Neymar 8 (Willian 71, 6); Fred 6.5
Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Jefferson, Dante, Maxwell, Henrique, Hernanes, Bernard, Jo, Maicon, Victor.
Wafungaji wa Magoli: Neymar 17, 34‘, Fred 49′, Fernandinho 84′
Idadi ya watazamaji: 69,112
Mchezaji bora wa mechi: Neymar
Mwamuzi: Jonas Eriksson (Sweden) 6.5
Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Jefferson, Dante, Maxwell, Henrique, Hernanes, Bernard, Jo, Maicon, Victor.
Wafungaji wa Magoli: Neymar 17, 34‘, Fred 49′, Fernandinho 84′
Idadi ya watazamaji: 69,112
Mchezaji bora wa mechi: Neymar
Mwamuzi: Jonas Eriksson (Sweden) 6.5
Neymar alifunga tena bao la pili katika dakika ya 34
Joel Matip (katikati) akishangilia bao lake la kusawazisha
dhidi ya Brazil.
CAMEROON 1-- 4 BRAZIL
Reviewed by habari motto
on
9:19 AM
Rating:
![CAMEROON 1-- 4 BRAZIL](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxzNppwoz8z7Ft-0su9TPEOc2Gw29GmI0BrWqpNABmtLVljkcJyLfKMifgSKQpjNk7DP2y1emDt5Z7OFqPC4rb_smNcgZnoXAAlDwmPh4q1SJdJnodyOJTF6l8FuPyjqI1uMUhqBSYvRpr/s72-c/NNEY.jpg)