BOKO HARAM Wajisalimisha Kwa IS

Boko Haram yasalimu amri kwa Is na ina maana gani kwa ulimwengu?
Kundi la wanamgambo wa kiislam la Islamic State limekubaliana na kiapo cha utii kutoka kwa kikundi cha Nigeria cha Boko Haram.
Kundi hilo limetoa mkanda wa video wenye ujumbe wake ,video hiyo inamuonesha mwanamume mmoja akizungumza kwa niaba ya kiongozi wa kundi lao , Abu Bakr al-Baghdadi,akikubaliana na kiapo cha utii kutoka kwa ndugu zao .
Mwanamume huyo anadai lengo lao ni kuanzisha na kusambaza Uhalifa Afrika Magharibi yote,na kudai kwamba maendeleo hayo ni habari njema .Ujumbe huo wa njia ya video bado hauja thibitishwa na kundi hilo.
Kundi la Boko Haram lilianza kampeni yake ya mashambulizi ya mabomu mnamo mwaka elfu mbili na tisa kama jaribio la kutaka kuusimika sharia katika eneo la Kaskazini mwa Nigeria na kukiri kiapo cha utii kwa kundi la Is kupitia ukurasa wa Twitter wa kundi la Is mwishoni mwa wiki iliyopita.BBC
BOKO HARAM Wajisalimisha Kwa IS BOKO HARAM Wajisalimisha Kwa IS Reviewed by habari motto on 8:04 AM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.