Hayo ndio yalikuwa majibu ya awali ya mbunge huyo wa Kigoma kaskazini alipokuwa akihojiwa na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam.
Mara baada ya mahakama kutoa uamuzi wake haraka mwanasheria mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Mh Tundu Lisu akazungumza na vyombo vya habari kuhusu Chadema kutomtambua Mh Zitto kama mwanachama wa chama hicho ambapo ili kusikia kauli ya Mh Zitto kuhusu suala hilo ITV ikafika katika ofisi ndogo za bunge zilizoko jijini Dar es Salaam na kumshuhudia Mh Zitto akiongoza vikao vya kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu ya mashirika ya uma PAC ambapo baada ya kumalizika kwa kikao hicho akazungumzia maamuzi hayo ya mahakama na Chadema baada ya kuhojiwa na waandishi wa habari.
Aidha kutokana na madai hayo Mh Zitto amesema kwa kuwa hana taarifa rasmi ijumaa ya wiki hii atakwenda jimboni kwake kuzungumza na wananchi wa jimbo lake kama mbunge na kisha jumanne ya wiki ijayo atahudhuria vikao vya bunge kama kawaida na kuongeza kuwa tukio hilo linamkomaza kisiasa na kwamba siasa zake ni zakujadili masuala na si watu kama walivyo baadhi ya wanasiasa wenzake.
Pia amezungumzia hatma ya mustakabali wake kisiasa na kuelezea mahusiano yake na chama cha demokrasia namaendeleo Chadema kwa sasa.
Source: ITV
Zitto Kabwe Asisitiza Kuwa Yeye ni Mbunge Halali wa Kigoma Kaskazini
Reviewed by habari motto
on
7:48 AM
Rating: