ARSENAL KIBOKO YAFUZU EUFA 2014

Mchezaji wa Arsenal(kushoto) akipambana na mchezaji wa Basiktas(kulia). Arsenal ilishinda 1-0

Asernal imefuzu kucheza fainali za kombe la UEFA kwa msimu wa 17 mfululizo baada ya kuichabanga Besiktas ya Uturuki kwa jumla ya goli 1-0.

Katika mchezo wa awali wiki moja iliyopita, timu hizo zilitoka sare ya kutofungana.

Hata hivyo, mchezaji mpya aliyejiunga na Arsenal msimu huu, Alexis Sanchez ndiye aliyeiwezesha Asernal kusonga mbele baada ya kufunga goli la kwanza tangu ajiunge na Arsenal akitokea Barcelona mwezi mmoja uliopita.

Sanchez aliyenunuliwa kwa kitita cha pauni milioni 35 kutoka Barcelona kwa kipindi chote cha mchezo alihaha kutafuta goli, ambapo katika dakika moja ya nyongeza katika kipindi cha kwanza cha mchezo aliweza kutumbukiza kimiani goli pekee kwa Arsenal na kufuzu kutoka hatua ya makundi kucheza fainali za UEFA kwa mwaka huu.

Arsenal ilipata nafasi za kumaliza mchezo mapema, lakini wachezaji wake Santi Cazorla na Alex Oxlade-Chamberlain walipoteza nafasi nyingi za wazi walizopata.

Zikiwa zimebaki dakika 15 kumaliza mchezo kipindi cha pili, Arsenal ilipata pigo baada ya mlinzi wake wa kulia Mathieu Debuchy alitolewa nje kwa kadi nyekundu kutokana na kuonyeshwa kadi mbili za njano. Lakini Arsenal waliendelea kupambana hadi dakika ya mwisho ya mchezo.

Timu nyingine zilizofuzu kucheza fainali za UEFA kwa mwaka huu katika michezo ya Jumatano usiku ni Athletic Bilbao iliyopata ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Napoli. (Jumla 4-2), Bayer 04 Leverkusen 4, FC Copenhagen 0, jumla(7-2).

Ludogorets Razgrad 1 - 0 Steaua Bucharest

Malmö FF 3 - 0 FC Red Bull Salzburg
ARSENAL KIBOKO YAFUZU EUFA 2014 ARSENAL KIBOKO YAFUZU EUFA 2014 Reviewed by habari motto on 10:31 AM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.