HUYU NDIYE ALIYEVUA NGUO KILELE CHA MLIMA MREFU DUNIANI



KIJANA Ben Boleyn aliamua kuvua nguo baada ya kufika kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro nchini chenye joto la kati ya sentigrade 10 hadi 12. Ben alifanya hivyo baada ya kuwekeana dau la shilingi 500 na mwenzake miongoni mwa aliopanda nao mlima huo.
Kijana huyo mwenye miaka 18 alipanda mlima huo katika kuchangisha fedha kusaidia watoto wa kituo cha kulea watoto cha Acorns Children's Hospice kilichopo jijini Worcester nchini
England.
Kwa kupanda mlima huo, Ben alikusanya pauni 600 ila baada ya kuvua nguo zake na kuweka picha yake mitandaoni alichangisha fedha nyingi zaidi.
Ben ambaye hujitolea katika kituo hicho alipanda futi 19,341 za Mlima Kilimanjaro kwa siku 9 akiwa na wenzake 7.Ben ambaye ni mwenyeji wa Kingswinford, England alisema: "Kila mtu alifurahia kitendo nilichokifanya katika kilele cha Mlima Kilimanjaro na kuchukua picha zangu.
"Wazazi wangu walipigwa na mshangao mwanzoni, ila walipoona watu wanazidi kuchangia kwa wingi walinielewa maana nilifanya kitu tofauti."


HUYU NDIYE ALIYEVUA NGUO KILELE CHA MLIMA MREFU DUNIANI HUYU NDIYE ALIYEVUA NGUO KILELE CHA MLIMA MREFU DUNIANI Reviewed by habari motto on 10:17 AM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.