Kilichotokea Jana Kuhusiana Na Benki Ya NBC



Nianze kuliandikia hili kwa kuonyesha furaha yangu kuwa huwenda sasa kumekua na uelewa juu ya maswala ya usalama mitandao. Nalisema hili kutokana na uhalisia kwamba Jana nilipata maswali kutoka kwa watu wengi sana huku nikipata jumbe nyingi zilizofanana zikielezea juu ya tukio la benk ya NBC kuingiliwa na wadukuzi
Wengi walinitaka pia nielezee huku nikiulizwa mbona hakuna nilichozungumza. Nilifarijika sana kwani muda uliopita wengi hawakua wakihoji juu ya maswala ya udukuzi pamoja na usalama mitandao na huwenda hii ilitokana na kutokua na uelewa wa maswala husika.NINI HASA KILITOKEA?Kwanza kabisa Kulikua na Itlafu ya Umeme ambayo ilisababisha baadhi ya Mashine kuzima.
Pili, Kulitokea Tahadhari ya Moto iliyosababisha wafanyakazi kuchuukua tahadhari ya kutoka nje.
Na Tatu, Mifumo ya Mobile banking (Inayotoa huduma za miamala kupitia simu za kiganjani) kushindwa kufanya kazi yake ipasavyo iliyo sababisha kutoa kiwango kisicho sawa kwa waliokua wakiangalia salio.
Matukio haya matatu yaliunganishwa na kutengeneza taarifa moja iliyo sambazwa kua kuna mdukuzi aliingilia banki ya NBC na kusababisha mifumo kutofanya kazi na hatimae kuhamisha kiasi kikubwa  cha pesa. Kitu ambapo kilipelekea wafanya kazi kutoka nje ili uchunguzi zaidi uweze kufanywa.Na anaepata taarifa anapo angalia salio anaona kunatatizo katika kiasi chake na kuamini jumbe ile. Panapotoka ufafanuzi wa taarifa hii wengi bado wanahoji bado kuna shaka niendelee kutoa ufafanuzi nini hasa kinaweza kikawa kimesababisha?NINI KINAWEZA KUWA TATIZO?
Wengi wanaweza kuhusisha matukio mawili ya mifumo kuzimika na mifumo ya Mobile money kutofanya kazi (Kuzidiwa nguvu) na kutoa taarifa zisizo sahihi na kinacho julikana kama "DDOS ATTACKS" ambapo pia ni uhalifu mtandao unaoweza kusababisha tukio la mifumo kuzima na kuzidiwa kufanya kazi.
Lakini pia ikumbukwe mifumo kuzima na wakati mwingine kushindwa kufanya kazi huwenda ni maswala tu ya kiufundi na isi husiane kabisa na uhalifu nilio uzungumzia.Panapo zimika kwa mitambo ya umeme wakati mwingine husababisha komputa kuzima ghafla kama mifumo ya kuhifadhia moto kutokua vizuri.Watu wengi wanapotuma maombbi kwenye mfumo wanaweza kuisababishia kushindwa kufanya kazi yake ipasavyo kutokana na kuzidiwa nguvu – Hii inafanana na aina ya uhalifu nilio uzungumzia ingawa huwenda ikawa ni wengi wametaka kwa nia njema kujua kiasi cha pesa zao baada ya kusikia kuna tatizo.Niendelee kuwasihi wa Tanzania, wanapo ona tatizo ni vizuri kulifatilia na kulichunguza kwa makini kabla ya kulitolea taarifa na pia kuwapongeza kwa dhati kwa kuweza kuchanganua mambo hadi kuweza kufikiria juu ya uhalifu mtandao ambapo ni  hatua nzuri ya uelewa wa maswala ya usalama mitandao nchini.
Aidha, Nimefahamishwa kua tayari taarifa kuhusiana na tukio hilo lilio ambatana na taarifa zilizo sambazwa limetolewa ufafanuzi na uongozi wa benki hiyo kwa wateja wake. Na Pia Nitafurahi sana kuona pakiwa na wa Tanzania wakiendelea kutaka kujuua zaidi kuhusiana na maswala ya usalama mitandao.


NA Yusuph Kileo
Kilichotokea Jana Kuhusiana Na Benki Ya NBC Kilichotokea Jana Kuhusiana Na Benki Ya NBC Reviewed by habari motto on 9:12 AM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.