Mtu mmoja amethibitishwa kufariki Dunia na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa vibaya baada ya moja ya Barabara iliyokuwa kwenye matengenezo kukatika katika mji wa Belo Horezonte karibu na eneo lenye shughuli nyingi la Lagoa da Pampulha,nchini Brazil.
Barabara hiyo ipo kilometa 3 kutoka Mineirao Stadium,uwanja uliotumika kwa mechi mbali mbali za kombe la dunia na utatumika kwenye nusu fainali ya Kombe la Dunia 2014.
Barabara hii ilikuwa ni moja ya kiungo kinachounganisha uwanja wa mpira na uwanja wa
Kimataifa wa Ndege. Barabara hiyo ni mpango wa mbasi ya mwendo kasi ambayo
ilisemekana ingekuwa tayari kutoa huduma wakati wa mashindano ya Kombe la Dunia.
Maafisa wa kikosi cha uokoaji nchini humo wakiendelea na kazi ya kuyanasua magari yaliyonasa baada ya kuangukiwa na Barabara hiyo,ambapo wamethibitisha kwamba Dereva wa basi hili ndie aliefariki Dunia katika tukio hilo la kuanguka kwa barabara hiyo ya Juu (Fly Over) kwenye mji wa Belo Horizonte,Brazil.
Kazi ikiendelea. Picha na AFP/Reuters