RAISI KABILA NDANI YA KASHFA NZITO TENA

Muungano wa wapinzani wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umemtuhumu Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo kuwa anakiuka haki za binadamu hususan waandishi wa habari.
Muungano huo ambao unajumuisha wapinzani wa kisiasa na kijamii wa serikali ya Kinshasa umekosoa vikali utendaji wa Rais Joseph Kabila na umemtuhumu kiongozi huyo kuwa ametenda jinai dhidi ya binadamu.
Muungano huo umeitaka jamii ya kimataifa kutayarisha mazingira ya kufikishwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kwa ajili ya kujibu mashtaka ya kutenda jinai ikiwa ni pamoja na kuua waandishi habari na wanaharakati wa masuala ya haki za binadamu.

RAISI KABILA NDANI YA KASHFA NZITO TENA RAISI KABILA NDANI YA KASHFA NZITO TENA Reviewed by habari motto on 11:48 AM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.