KALI KULIKO ZOTE: NA HUU NI UZINDUZI WA NANI KAMA MAMA YA CHRISTIAN BELLA.


Mashabiki wakimtunza Bella baada ya kuwakuna. 
MKALI wa muziki wa dansi hapa nchini, Christian Bella, Jumamosi usiku alizindua albam yake ya ‘Nani Kama Mama’ ambapo umati mkubwa wa mashabiki ulijitokeza kwenye onesho hilo lililofanyika Ukumbi wa Mzalendo Pub, Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.

Katika onesho hilo Bella alisindikizwa na Bendi yake ya Malaika Musica pamoja na wanamuziki wa kizazi kipya, Ommy Dimpoz, Banana Zorro na Matonya. Ingawa mvua ilitaka kuharibu mambo kwenye eneo hilo lililokuwa wazi, mashabiki waliofurika ukumbini hapo walikomaa mwanzo mpaka mwisho.
Bella na Banana wakikamua.
 
Matonya akitoa sapoti kwa vibao vyake kikiwemo cha 'Vailet'.
 
Ommy Dimpoz akikamua.
 
Mashabiki wakijimwaya.
 
Bella akikamua.
 
Papaa Thom Diamond, akimmwagia Ommy Dimpoz noti nyekundu.
 
Bella baada ya kuwaambia mashabiki anayempenda mama yake anyooshe mkono juu.
 
Mashabiki wakijifunika kava za viti baada ya mvua kuanza kutibua mambo.
 
Bella na Ommy Dimpoz wakiimba kibao cha ‘Nani Kama Mama’.
 
STORI/PICHA NA: RICHARD BUKOS / GPL  

KALI KULIKO ZOTE: NA HUU NI UZINDUZI WA NANI KAMA MAMA YA CHRISTIAN BELLA. KALI KULIKO ZOTE: NA HUU NI UZINDUZI WA NANI KAMA MAMA YA CHRISTIAN BELLA. Reviewed by habari motto on 6:19 PM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.