Msanii bora wa muziki wa Reggae na Ragga Tanzania, DABO amepata nafasi ya kuipeperusha bendera ya Tanzania katika anga za kimataifa, baada ya kuchaguliwa kuwania tuzo kubwa kabisa za muziki za International Reggae and World Music.
DABO anawania tuzo hizi katika kipengele cha Mtumbuizaji Mpya Bora, akikabiliwa na ushindani kutoka kwa wasanii MC Norman kutoka Uganda, Alkaline na Kranium kutoka Jamaica, Shatta Wale wa Ghana na mjukuu wa Bob Marley ambae ni Daniel Bambatta Marley.
Zoezi la kuwapigia kura wasanii hawa kuwawezesha kushinda linaendelea sasa mtandaoni.