Kugombana ni jambo ambalo halikwepeki katika uhusiano wa kimapenzi. Upo ugomvi
ambao ni wa kawaida na huisha kirahisi lakini upo ugomvi ambao huwa mkubwa na kama
ukitokea na ukashindwa kujua nini cha kufanya kuweka mambo sawa, husababisha ufa
kwenye penzi lenu.Leo tutazungumzia mambo muhimu ya kufanya inapotokea wewe na
mpenzi wako mmeingia katika ugomvi mkubwa, mmetoleana maneno machafu au hata
kupigana.
1. TAFAKARI CHANZO CHA TATIZO
Kuna usemi kwamba ukitaka kulitatua vizuri tatizo ni lazima kwanza ujue chanzo cha tatizo
lenyewe. Ukishindwa kugundua chanzo cha tatizo, basi na wewe unakuwa sehemu ya tatizo.
Utashangaa kwamba wapenzi wengi hugombana na mambo kuwa makubwa kabisa kwa
sababu ya vyanzo vidogo ambavyo walishindwa kuvigundua mapema na matokeo yake vikazaa matatizo
mengine.
Mfano rahisi, chanzo kinaweza kuwa mpenzi wako amekupigia simu lakini ukashindwa
kuipokea kwa muda muafaka. Atakapopiga kwa mara nyingine au mkikutana, usitegemee
atakufurahia kwa sababu atahisi umemdharau kwa kutopokea simu yake.Endapo ukifanya
makosa ya kushindwa kuliona kosa lako mapema na kushindwa kuomba radhi au kutoa
maelezo yanayoeleweka kwa nini hukupokea simu, matokeo yake utamjibu vibaya, naye
atakujibu vibaya na mwisho mtaishia kupigana au kuachana kabisa mkiwa mmeshatoka
kabisa kwenye kosa la msingi.
Bila shaka msomaji wangu umeona jinsi chanzo kidogo kinavyoweza kusababisha tatizo
kuwa kubwa. Ndoa nyingi au uhusiano unaofika mwisho huwa umesababishwa na mambo
madogo ambayo yalishindwa kutafutiwa suluhu mapema.
Katika kila ugomvi unaotokea, jambo la kwanza jipe muda wa kutafakari chanzo
kilichosababisha mkagombana. Wakati mwingine wewe ndiyo unaweza kuwa chanzo cha
tatizo lakini kama ukiyajua makosa yako mapema na kukiri kisha kuomba radhi kwa
mwenzio, utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kurudisha mapenzi kwa haraka.
2. MPE MUDA HASIRA ZIISHE
Kila binadamu ameumbwa akiwa na hasira na kwa bahati mbaya ni wachache wanaoweza
kuzidhibiti hasira zao. Ni rahisi mtu kutukana, kupiga au kuharibu vitu akiwa na hasira.
Baada ya kugombana, kila mmoja lazima atakuwa na hasira na njia pekee inayoweza
kuepusha matatizo zaidi, ni kujipa muda na kumpa muda mwenzako ili hasira zipungue.
Kama mpo sebuleni na umetokea ugomvi, ni busara kwenda chumbani au nje mpaka hasira
zako zikiisha. Ni makosa kulazimisha suluhu wakati kila mmoja akiwa na jazba kwani
mtaishia pabaya zaidi.
Ukishaona hasira zako zimetulia na mwenzako naye ametulia, unaweza kuanzisha mada
mengine.
Mfano rahisi, chanzo kinaweza kuwa mpenzi wako amekupigia simu lakini ukashindwa
kuipokea kwa muda muafaka. Atakapopiga kwa mara nyingine au mkikutana, usitegemee
atakufurahia kwa sababu atahisi umemdharau kwa kutopokea simu yake.Endapo ukifanya
makosa ya kushindwa kuliona kosa lako mapema na kushindwa kuomba radhi au kutoa
maelezo yanayoeleweka kwa nini hukupokea simu, matokeo yake utamjibu vibaya, naye
atakujibu vibaya na mwisho mtaishia kupigana au kuachana kabisa mkiwa mmeshatoka
kabisa kwenye kosa la msingi.
Bila shaka msomaji wangu umeona jinsi chanzo kidogo kinavyoweza kusababisha tatizo
kuwa kubwa. Ndoa nyingi au uhusiano unaofika mwisho huwa umesababishwa na mambo
madogo ambayo yalishindwa kutafutiwa suluhu mapema.
Katika kila ugomvi unaotokea, jambo la kwanza jipe muda wa kutafakari chanzo
kilichosababisha mkagombana. Wakati mwingine wewe ndiyo unaweza kuwa chanzo cha
tatizo lakini kama ukiyajua makosa yako mapema na kukiri kisha kuomba radhi kwa
mwenzio, utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kurudisha mapenzi kwa haraka.
2. MPE MUDA HASIRA ZIISHE
Kila binadamu ameumbwa akiwa na hasira na kwa bahati mbaya ni wachache wanaoweza
kuzidhibiti hasira zao. Ni rahisi mtu kutukana, kupiga au kuharibu vitu akiwa na hasira.
Baada ya kugombana, kila mmoja lazima atakuwa na hasira na njia pekee inayoweza
kuepusha matatizo zaidi, ni kujipa muda na kumpa muda mwenzako ili hasira zipungue.
Kama mpo sebuleni na umetokea ugomvi, ni busara kwenda chumbani au nje mpaka hasira
zako zikiisha. Ni makosa kulazimisha suluhu wakati kila mmoja akiwa na jazba kwani
mtaishia pabaya zaidi.
Ukishaona hasira zako zimetulia na mwenzako naye ametulia, unaweza kuanzisha mada
juu ya kilichosababisha mkagombana. Tumia lugha ya upole kwani endapo utakuwa
ukifoka au
kuzungumza kwa sauti ya juu, matokeo yake mtarudia tena kugombana.
3. MPE NAFASI YA KUZUNGUMZA
Huwezi kumuelewa mtu kabla hujampa nafasi ya kuzungumza na kumaliza kile
alichokusudia kukisema. Endapo tatizo limetokea na upo kwenye hatua za kusaka suluhu,
mpe mwenzako nafasi ya kueleza dukuduku lililopo ndani ya moyo wake.
Usimkatishe wala kumbishia
chochote, muache aongee ulichomuudhi mpaka dukuduku lake liishe kisha na wewe jieleze
kwa upole na sauti tulivu.
4. OMBA MSAMAHA
Hakuna silaha nzuri inayoweza kukusaidia kuushinda ugomvi wowote na kutuliza mambo
kabla hayajawa mabaya kama kuomba msamaha. Neno ‘samahani’ ni dogo lakini lina maana
3. MPE NAFASI YA KUZUNGUMZA
Huwezi kumuelewa mtu kabla hujampa nafasi ya kuzungumza na kumaliza kile
alichokusudia kukisema. Endapo tatizo limetokea na upo kwenye hatua za kusaka suluhu,
mpe mwenzako nafasi ya kueleza dukuduku lililopo ndani ya moyo wake.
Usimkatishe wala kumbishia
chochote, muache aongee ulichomuudhi mpaka dukuduku lake liishe kisha na wewe jieleze
kwa upole na sauti tulivu.
4. OMBA MSAMAHA
Hakuna silaha nzuri inayoweza kukusaidia kuushinda ugomvi wowote na kutuliza mambo
kabla hayajawa mabaya kama kuomba msamaha. Neno ‘samahani’ ni dogo lakini lina maana
kubwa kwa yule mtu anayelitoa na anayelipokea.
Hata kama unaona dhahiri kwamba kosa siyo lako, omba msamaha kwanza kisha baada ya
hapo anza kumuelewesha mpenzi wako kwa upole. Lazima mwisho na yeye atayaona
makosa yake na kukuomba msamaha, mtaweza kuepuka kuukuza ugomvi huo na
kurudisha hisia za mapenzi.
5. USIWEKE KINYONGO
Endapo umeamua kuomba msamaha kwa mpenzi wako, au yeye amekuomba msamaha,
samehe kwa dhati kutoka ndani ya moyo wako na sahau kile kilichotokea. Ni kosa kubwa
kuweka kinyongo rohoni, yaani unamwambia kwamba umemsamehe wakati moyo wako
bado una hasira naye. Ukisamehe kwa dhati, jifunze na kusahau kwani kusamehe
kunaenda sambamba na kusahau.
Wazungu wanasema forgive and forget. Elewa kwamba mpenzi wako ni binadamu ambaye
hajakamilika, wala si malaika.
Lazima atakuwa akikosea mara kwa mara, endapo utakuwa ukilimbikiza vinyongo, unafuga
matatizo makubwa kwani siku nyingine akikukosea hata jambo dogo, utakumbushia na ya
jana na juzi na mwisho ugomvi utakuwa mkubwa sana.
Kwa maoni, ushauri au swali nicheki kwa namba za hapo juu.
Hata kama unaona dhahiri kwamba kosa siyo lako, omba msamaha kwanza kisha baada ya
hapo anza kumuelewesha mpenzi wako kwa upole. Lazima mwisho na yeye atayaona
makosa yake na kukuomba msamaha, mtaweza kuepuka kuukuza ugomvi huo na
kurudisha hisia za mapenzi.
5. USIWEKE KINYONGO
Endapo umeamua kuomba msamaha kwa mpenzi wako, au yeye amekuomba msamaha,
samehe kwa dhati kutoka ndani ya moyo wako na sahau kile kilichotokea. Ni kosa kubwa
kuweka kinyongo rohoni, yaani unamwambia kwamba umemsamehe wakati moyo wako
bado una hasira naye. Ukisamehe kwa dhati, jifunze na kusahau kwani kusamehe
kunaenda sambamba na kusahau.
Wazungu wanasema forgive and forget. Elewa kwamba mpenzi wako ni binadamu ambaye
hajakamilika, wala si malaika.
Lazima atakuwa akikosea mara kwa mara, endapo utakuwa ukilimbikiza vinyongo, unafuga
matatizo makubwa kwani siku nyingine akikukosea hata jambo dogo, utakumbushia na ya
jana na juzi na mwisho ugomvi utakuwa mkubwa sana.
Kwa maoni, ushauri au swali nicheki kwa namba za hapo juu.
FUATA MBINU HIZI KURUDISHA MAPENZI KWA MPENZI WAKO
Reviewed by habari motto
on
7:49 AM
Rating: