NA HIVI NDIVYO KLABU ZA ENGLAND ZILIVYOFANYA KUFURU YA USAJILI MSIMU HUU

Am I worth it? Angel di Maria was the most expensive acquisition after joining United for a record £59.7m


Mimi ni bosi wao? Angel di Maria amekuwa mchezaji aliyenunuliwa kwa bei mbaya zaidi kihistoria Uingereza baada ya Manchester United kulipa Pauni Milioni 59.7 Real MadridMESOTHELIOMA LAW FIRM 
DONATE CAR TO CHARITY CALIFORNIA 
DONATE CAR FOR TAX CREDIT 

 KLABU za Ligi Kuu ya England zimetumia Pauni Milioni 858 baada ya dirisha la usajili msimu huu kufungwa, ambayo ni zaidi ya kiasi kilichotumika kwa klabu za La Liga ya Hispania (Pauni Milioni 425), Serie A ya Italia (Pauni Milioni 260) na Ligue 1 ya Ufaransa (Pauni Milioni 100) jumla.

Hii imeipiku hata Ujerumani ambako klabu zilipoamua kuingia sokoni kwa fujo Bundesliga zilitumia Pauni Milioni 250 jumla pamoja na Pauni Milioni 100 kwa awamu moja ya usajili.

Sehemu kubwa ya fedha inatokana na mikataba ya Televisheni England ambayo inazipa jeuri klabu kusajili kwa bei kubwa na kulipa mishahara minono wachezaji. 



Chati hii inaonyesha namna klabu zilivytumia fedha kusajili Ulaya, Ligi Kuu England ikiongoza kwa kutumia Pauni Milioni 857.68

FEDHA NYINGI ZIMEKWENDA KWA WACHEZAJI WA KIGENI
Katika kiasi hicho cha jumla cha fedha, klabu za Ligi Kuu ya England zimetumia Pauni Milioni 520.8 kusajili wachezaji wa kigeni, yaani kutoka née ya Uingereza  (England, Scotland and Wales). 

DILI ZA BEI CHAFU ZAIDI USAJILI HUU ENGLAND

Angel Di Maria [Real Madrid - Manchester United] Pauni Milioni 59.7
Alexis Sanchez [Barcelona - Arsenal] Pauni Milioni 35
Diego Costa [Atletico Madrid - Chelsea] Pauni Milioni 32
Eliaquim Mangala [FC Porto - Manchester City] Pauni Milioni 32
Cesc Fabregas [Barcelona - Chelsea] Pauni Milioni 30
Ander Herrera [Athletic Bilbao - Manchester United] Pauni Milioni 29
Romelu Lukaku [Chelsea - Everton] Pauni Milioni 28
Luke Shaw [Southampton - Manchester United] Pauni Milioni 27 (inaweza kupanda hadi Milioni 31)
Adam Lallana [Southampton - Liverpool] Pauni Milioni 25
Dejan Lovren [Southampton - Liverpool] Pauni Milioni 20
Lazar Markovic [Benfica - Liverpool] Pauni Milioni 20
City slicker: Eliquiam Managal arrived from Porto for £32m


Top Gun: Alexis Sanchez was the second costliest transfer for £35m
Dau kubwa: Usajili wa Eliquiam Mangala (City) na Alexis Sanchez (Arsenal) ump kwenye rekodi ya usajili wa bei mbaya
Blues brother: Cesc Fabregas joined Chelsea from Barcelona


Super striker: Jose Mourinho brought in Diego Costa early
Pacha wa Blues: Chelsea imefanya biashara ya maana kuwasajili Cesc Fabregas (kushoto) na Diego Costa (kulia)

KLABU IPI IMEFANYA USAJILI BORA?
Manchester United imetumia (jumla ya Pauni Milioni 153.1), na Stoke imetumia (Pauni Milioni 3.4) wakati Southampton imetengeneza faida ya Pauni Milioni 30.7 katika usajili wake.
Chelsea imefanya biashara nzuri yenye thamani halisi ya vipengele vya fedha, ikitengeneza faida na kuboresha timu. Na Leicester na Southampton pia zimefanya vizuri katika thamani halisi kwa kutengeneza timu nzuri kwa gharama kidogo.
Wachezaji walionunuliwa ni pamoja na makipa saba, mabeki 36, viungo 37 na washambuliaji 23
MESOTHELIOMA LAW FIRM 
DONATE CAR TO CHARITY CALIFORNIA 
DONATE CAR FOR TAX CREDIT 
NA HIVI NDIVYO KLABU ZA ENGLAND ZILIVYOFANYA KUFURU YA USAJILI MSIMU HUU NA HIVI NDIVYO KLABU ZA ENGLAND ZILIVYOFANYA KUFURU YA USAJILI MSIMU HUU Reviewed by habari motto on 8:53 AM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.