Kamishna wa zamani wa mji wa Dar es Salaam aaga dunia

Image result for Abbas Kandoro
Aliyekuwa kamishna wa eneo la Mbeya na mji wa Dar es Salaam Abbas Kandoro ameaga dunia katika hospitali kuu ya Muhimbili (MNH).
Habari hizo zilithibitishwa na msemaji wa hospitali hiyo Aminiel Aligaesha.
Bwana Kandoro alifariki siku ya Ijumaa, Aprili 27, 2018 wakati alipokuwa akipata matibabu.
Alifariki katika hospitali hiyo siku hiyohiyo aliyolazwa.
Kulingana na familia yake maombi ya mwisho ya marehemu yatafanyika katika msikiti wa Manyema uliopo Kariakoo mjini Dar es Salaam ambapo waombolezaji watakuwa na fursa ya mwisho kuuaga mwili.
Mwili wake baadaye utasafirishwa hadi mjini Iringa kwa mazishi kulingana na ripoti za gazeti la The Citizen Tanzania.
Image result for Abbas Kandoro
Rais John Pombe Magufuli alituma salamu za rambirambi kwa familia ya Kandoro . Raisi Magufuli amesema kuwa ameshangazwa na kifo cha marehemu, akisema kuwa mchango wake katika kubadili sekta ya huduma za umma utakumbukwa.
Kabla ya kifo chake, marehemu alikuwa amehudumu katika afisa tofauti za umma kama kamishna na mkuu wa wilaya ya Tabora , Arusha , mwanza na Mbeya 
NA BBC
Kamishna wa zamani wa mji wa Dar es Salaam aaga dunia Kamishna wa zamani wa mji wa Dar es Salaam aaga dunia Reviewed by habari motto on 6:22 AM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.